EATV
NA EA RADIO KUWALETA P SQURE NCHINI
Na
Mwanne Othman
Wasanii
wakali na machachari Africa ambao ni Mapacha Peter na Paul maarufu
' P Squre' wanatarajiwa kuja nchini Tanzania na kufanya shoo kali na
kabambe jijini Dar es Salam mnamo tarehe 23 Mwezi wa 11 mwaka huu
2013.
Akizungumza
na waandishi wa Habari kwenye ukumbi wa Hoteli ya Hyatt Regency
zamani Kempiski jijini Dar es Salaam Mtangazaji wa East Africa
Television pamoja East Africa Radio ambao ndio waratibu wa Tamasha
hilo, Hilaly Daudi maarufu Zembwela alisema kuwa lengo kubwa la
kuwaleta wanamuziki hao wanaoongoza kwa umaarufu kila kona Duniani ni
kutoa Burudani na Somo kwa wanamuziki wa Tanzania kwa namna ambavyo
muziki unaweza kufanyika katika hali tofauti na waliyozoea.
![]() |
p squre wakiwa katika pozi |
![]() |
Mapacha wawili wakiwa katika pozi |
Zembwela
alisema Tamasha hilo litakuwa ni la moja kwa moja kutoka kwenye ala
ambapo kwa lugha ya Kigeni tunaita Live Band na jumla ya wanamuziki
13 wataambatana na P squre kufanya shoo hiyo.
“P
squre watafanya onesho masaa mawili mfululizo bila kupumzika na
kutakuwa na wasanii wa kuwasindikiza ambao tutakuwa tunawatangaza
kadri muda utakavyozidi kukaribia “ alisema Zembwela.
Tamasha
hilo la Kihistoria limedhaminiwa na Kampuni ya Vodacom Tanzania ambao
wamekuwa wa kwanza kuonesha ushirikiano katika hilo na wamekubaliana
na Waratibu ambao ni EATV na East Africa Radio kuifanikisha Burudani
hiyo kubwa na ya aina yake.
No comments:
Post a Comment
Tafadhali Ndugu Msomaji Zingatia Kutumia Maneno mazuri na ya busara kwa Faida ya Wasomaji Wengine