MAJARIBIO BLOG

Thursday, October 10, 2013

MSICHANA ACHANWA VIWEMBE USONI, MWILINI

 KISA...................... SOMA HABARI KAMILI

NA MWANNE OTHMAN

Msichana wa kazi katika nyumba moja iliyopo Mbagala kwa Mangaya anayefahamika kwa jina la Sailis Mapunda mwenye umri wa miaka 18 amejeruhiwa vibaya kwa Viwembe na wanawake wawili ambao wanaosemekana kuwa ni mtu na mke mwenzie, imefahamika.

Akizungumza Mwanne Othman huko nyumbanin kwao Mbagala kwa Mangaya, Sailis alisema kuwa wanawake hao alikutana nao njiani akitokea dukani kununua mkate ambao walimsimamisha na kumuuliza kuwa wewe ndo Salome na kuwajibu haha kwamba yeye si Salome.


SAILIS AKIWA AMEUMIA USONI BAADA YA KUPIGWA KWA  MADAI YA KUSINGIZIWA SKENDO


Alisema wanawake hao hawakutaka kumuamini Sailis hivyo waliendelea kumsakama na kumtuhumu kwamba ndo Salome anayewachukulia mume wao na kuanza kumvamia mmmoja akimpiga na mwengine kumkata VIWEMBE katika sehemu mbalimbali za mwili ikiwemo Usoni karibu kabisa na Jicho, Mgongoni pamoja na Mikononi hatimaye kumsababishia maumivu makali.

Sailis alisema wanawake hao ambao ambao majina yao yapo kapuni  wakiwa na umri kati ya miaka 24 na 25 kwamba hawajui na hakuwahi kukutana nao awali.

Mpaka sasa kesi iko kwenye Vyombo vya Dola.


HAPA AKIWA NA SHANGAZI YAKE PAMOJA NA DADA ZAKE.

No comments:

Post a Comment

Tafadhali Ndugu Msomaji Zingatia Kutumia Maneno mazuri na ya busara kwa Faida ya Wasomaji Wengine