MAJARIBIO BLOG

Thursday, October 10, 2013

KHADIJA KOPA EDA JUMAPILI

NA MWANE OTHMAN
KHADIJA KOPA AKIWA STEJINI AKIFANYA VITU VYAKE


KHADIJA KOPA KUTOKA EDA

Mwimbaji wa muziki wa taarab ya Kisasa maarufu Malikia wa Mipasho Khadija Omar Kopa anatarajia kutoka Eda Tarehe 13 mwezi huu wa 10, sawa na siku ya Jumapili huko nyumbani kwa Marehemu Mumewe Jafar Ally Bagamoyo.

Akizungumza na Mwanne Othman kwa njia ya simu Khadija Kopa alisema anatarajia kumaliza eda yake hiyo siku ya tarehe 13 lakini nje atatoka rasmi siku ya tarehe 14 yaani Jumatatu ijayo ambapo alisema angependa kusomewa Dua ili Mwenyezi Mungu amzidishie Moyo wa Iman.


KHADIJA KOPA SIKU ALIYOFIWA NA MUMEWE


Khadija Kopa alikuwan ndani kwa Takriban miezi minne na siku 10 baada ya kufiwa na mumewe aliyekuwa Diwani wa Kata ya Magomeni Wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani ambapo alifariki dunia mnamo mwishoni mwa mwezi wa tano akisumbuliwa na maradhi ya malaria na alizikwa katika makaburi yaliyopo Magomeni wilaya ya Bagamoyo Mkoani humo, huku akimuacha Mkewe Kipenzi Khadija Kopa kwenye EDA, akiwa katika wakati Mgumu wa kumkosa mumewe kipenzi.


No comments:

Post a Comment

Tafadhali Ndugu Msomaji Zingatia Kutumia Maneno mazuri na ya busara kwa Faida ya Wasomaji Wengine