MAJARIBIO BLOG

Monday, March 31, 2014

NJIA 64 ZATARAJIWA KUFUTWA DAR

Na Mwanne Othman


Baadhi ya madereva wa daladala jijini Dar es Salaam wamesema hatua inayotarajiwa kufanyika ya kufutwa kwa njia 64 za daladala ili kupisha mradi wa mabasi yaendayo kasi jijini Dar es Salaam, itawaathiri kwa kisasi kikubwa kikazi kwani asilimia kubwa ya abiria hupatikana katika njia hizo, Ea Drive imezungumza nao.

Nilizungumza na Mshauri Elekezi wa mabasi yaendayo kasi jijini Dae es Salaam ndugu Felix Mlaki ambaye naye kwa upande wake alielezea mpango mzima uliosababisha hatua hiyo kufikiwa ni kwamba lengo ni kutoa nafasi kwa mabasi hayo pindi yatakapoanza na madaladala yatapatiwa njia mbadala kutoka SUMATRA.

Aidha alisema wananchi watarajie kutopata usumbufu katika safari zao kwani wana mfumo mzuri katika ununuzi wa tiketi unaweza kununua tiketi ya hata ya wiki nzima, na kufika safari yake bila kuchelewa

Akizungumzia juu ya nauli ya usafiri huo alisema kuwa wapo katika mchakato wa kukokotoa na utakapomalizika mchakato huo watatoa taarifa kamili.

Ndugu Mlaki akizitaja barabara hizo zitakazoathirika ni pamoja na Kariakoo Mwenge, Posta Mwenge, Ubungo Kariakoo, Mbezi na kadhalika.







No comments:

Post a Comment

Tafadhali Ndugu Msomaji Zingatia Kutumia Maneno mazuri na ya busara kwa Faida ya Wasomaji Wengine