MAJARIBIO BLOG

Friday, April 11, 2014

IJUE HISTORIA FUPI YA JUMA BHALO

Na Mwanne Othman
Tam Tam za Mwambao
Aprili 13/2014
Jumapili
Saa 4:00 asb12:00 mchana
KIFO CHA JUMA BHALO

Msanii Mkongwe katika tasnia ya muziki wa Taarab asilia mwenye asili ya Mombasa ambaye pia alikuwa mwenye uwezo wa kutunga mashairi, kuimba huku akipigia kinanda Mohammed Khamis Juma Bhalo maarufu kama Profesa Juma Bhalo leo ametimia siku ya 7 toka kufa kwake, ambapo alifariki mnamo tarehe 5/4/2014 na kuzikwa Jumapili tarehe 6/4/2014.

mwa4othman.blogspot.com ilizungumza na mtoto wa mwisho yaani Kitinda Mimba wa marehemu Profesa Juma Bhalo anayefahamikia kwa jna la Ahmed Juma kwa njia ya simu kutoka Mombasa, ambaye  alisema alifariki baada ya kuugua kwa muda mfupi, na alizikwa kwenye makaburi ya Kikoani.

Tumsikilize Ahmed Juma Bhalo akitupatia historia fupi ya Marehemu baba yake.

Tam Tam Clip 5(Sikiliza Tam Tam za Mwambao Jumapili tarehe 13/4/2014

Akizungumzia juu ya mtoto ambaye ameweza kufata nyayo za baba yake Profesa Juma Bhalo alisema ilikuwa vigumu sana kwa baba yake kukubali mwanaye kufata nyayo zake japokuwa baadaye alimkubalia miongoni mwa wanawe hao kufata nyayo hizo, Tumsikilize, pamoja na kufahamu pia asili hasa marehemu Juma Bhalo.
 

DONDOO MUHIMU
-Alizaliwa mwaka 1940 mtaani shela eneo la malindi katika Pwani ya Kenya

Na amefariki akiwa na umri wa miaka 74 , na kutokana na hali ya maisha ya wazazi wake hakuweza kuendelea na masomo hivyo aliishia darasa la 4 na kuendeleza masomo ya madrasa, lakini pia hakuweza kumaliza masomo hayo kutokana na ugumu wa hali ya maisha pia.

Ameacha wajane wawili, watoto 14 japokuwa alibahatika kupata watoto 17 lakini watatu wametangulia mbele ya haki.

Alianza kuimba Mwaka1957, na 1mwaka 1966 alianzisha kikundi chake kilichoitwa Bhalo and Party huku akisaidiana na Malenga wa Mvita.
Alikuwa na uwezo wa kukariri nyimbo za Kihindi na kuziimba

Imeandaliwa  na Mwanne Othman:
Mtangazaji wa Taarab east africa radio.

MAREHEMU PROFESA JUMA BHALO ENZI YA UHAI WAKE
 



No comments:

Post a Comment

Tafadhali Ndugu Msomaji Zingatia Kutumia Maneno mazuri na ya busara kwa Faida ya Wasomaji Wengine