Na Mwanne Othma
14/4/2014
Halmashauri ya Manispaa ya
Kinondoni imewataka wahanga wote wa mafuriko walioweka makazi yao
katika Vituo vya mradi wa mabasi yaendayo kasi waondoke katika maeneo
hayo.
Akizungumza na
mwa4othman.blogspot.com, Msemaji wa Manispaa ya Kinondoni Ndugu
Sebastian Mhohela alisema wahanga wote wanatakiwa kuripoti katika
ofisi za Mtendaji kata ili kupata maelekezo wapi waende.
Aidha Akizungumzia juu ya
Maafa na madhara yaliyopo katika Manispaa ya Kinondoni yaliyotokana
na mvua hizo alisema tayari idadi ya vifo vimeshafikia watu 24,
miundo mbinu imeathirika kwa kiasi kikubwa kama maraja kuvunjika
barabara kubomoka, na hata wanafunzi kukosa masomo kutokana na baadhi
ya mashule kujaa maji.
mwa4othman.blogspot.com,
ilizungumza na wahanga hao ambao nao waliiomba serikali kuwasaidia
badala ya kutoa kauli za kuwataka kuondoka maeneo hayo.
Katika hatua nyingine
mlezi wa Chama Cha Mapinduzi na Mchumi
wa tawi la tambaza ambaye
pia ni mtoto wa Waziri wa Jinsia Wanawake na watoto Mh. Sofia
Simba, aliyefahamika kwa jina Aladin ambaye alifika mahali hapo
kuwapatia msaada wahanga hao kama maji, soda, mikate, mchele na
kadhalika, alitoa wito kwa Serikali kuwatengenezea mazingira mazuri
wahanga hao kwa kudhibiti mkondo wa maji ili waweze kuendeleza maisha
yaoNaye
Mtangazaji
wa east africa radio Mwanne Othman aliyeoneshwa kuguswa na hali ya
wahanga hao hususan watoto wasio na hatia kupata tabu, hivyo aliamua
kuwapelekea vitafunwa kama vile Mikate, Maandazi, Keki na kadhalika.
No comments:
Post a Comment
Tafadhali Ndugu Msomaji Zingatia Kutumia Maneno mazuri na ya busara kwa Faida ya Wasomaji Wengine