MAJARIBIO BLOG

Friday, May 16, 2014

DAWASCO KUWASAKA WAHUJUMU WAO

Na Mwanne Othman

15/5/2014


Shirika la maji safi na maji taka Dawasco limefanikiwa kukamata zaidi ya watu watano katika oparesheni yake iliyoanza jana inayolenga kuwasaka wahujumu wa shirika hilo wanaojiunganishia maji kinyume na sheria.

Akizungumza na mwanneothman.blogspot.com, Msemaji wa Dawasco Everlasting Lyaro amesema oparesheni hiyo ni kuduma na kusema wamesikitishwa na mbinu walizogundua jinsi mtu mmoja anavyoweza kudhulumu haki za wenzake za kukosa maji takriban miezi mitatu.

Aidha Bi Everlasting ametoa wito kwa wananchi kuonesha ushirikiano kwa Dawasco kwa kutoa taarifa pindi wanapoona kuna mtu anakwenda kinyume na sheria katika kuhujumu Shirika hilo, pamoja na kuanisha vitu walivyokama kama wahujumu hao na kutolea mfano kuwa huu ni ujangili pia, kwani ujangili si kwa wanyama pori pekee hata wahujumu maji wanawahesabia pia ni majangili.


No comments:

Post a Comment

Tafadhali Ndugu Msomaji Zingatia Kutumia Maneno mazuri na ya busara kwa Faida ya Wasomaji Wengine