MAJARIBIO BLOG

Monday, May 19, 2014

VIJANA JIHUSISHENI KATIKA CHAGUZI ZA SERIKALI

Na Mwanne Othma

Vijana nchini wametakiwa kutambua umuhimu wa kushiriki katika chaguzi ndogo hususan chaguzi za Serikali za Mtaa ili kujiongezea uelewa zaidi katika kufahamu mambo muhimu yanayoambatana na chaguzi hizo.

Akizungumza na Drive Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mwananyamala kwa Kopa ndugu Juma Mbilinga amesema vijana wengi na hata baadhi ya Wazee wamekuwa wakidharau chaguzi za Serikali za Mitaa bila kujali kwamba Serikali huanzia katika ngazi hiyo.

Aidha Drive ilizungumza na Vijana wenyewe iwapo wana uelewa na kufahamu umuhimu wa kushiriki katika chaguzi ndogo ndogo hususan Serikali za mitaa ambapo walisema changamoto ya maeneo ya kupigia kura, uchache wa vifaa hali inasababisha kijana kukaa muda mrefu kusubii kupiga kura huchangia vijana kutoshiriki kikamilifu..

Kadhalika tulizungumza na Mama Ukoko Zigo kama mzazi akizungumzia iwapo wazazi wanachangia kuwazuia watoto wao kutoshiriki katika harakati hizo za uchaguzi ambae nae kwa upande wake alisema yuko katika mstari wa mbele katika kuwahamasisha vijana kushiriki.




No comments:

Post a Comment

Tafadhali Ndugu Msomaji Zingatia Kutumia Maneno mazuri na ya busara kwa Faida ya Wasomaji Wengine