MAJARIBIO BLOG

Wednesday, May 21, 2014

WAZIR FENERA I AWASIHI WASANII KUJALI AFYA ZAO

Na Mwanne Othman

Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo Mh. Feneral Mukangara amewaomba wasanii wa tasnia ya filamu nchini wasimamie kazi zao ipasavyo kuhakikisha wanajijengea mfumo chanya katika kazi zao, huku wakijewekea utaratibu wa kwenda hospitali kuangalia afya zao ili kujiepusha na magonjwa nyemelezi.

Mh. Waziri Fenera ameyasema hayo jana katika viwanja vya leaders klabu katika shuhuli za kuagwa kwa msanii wa filam Adam Philip Kuambiana ambaye amezekwa leo mchana katika makaburi ya Kinondoni.

Aidha akijibu swali la mmoja wa wasanii anayefahamika kwa jina la Dr. Cheni la kuomba wasanii wa filamu kutengewa eneo ama kiwanja chao maalum cha kuzikiwa ambapo alisema.

Waziri Habari Vijana Utamadunin na Michezo



Mh. Waziri Mukangara akiwasili katika viwanja vya leader club wakati wa shuhuli za kuaga mazishi ya marehem Adam Kuambiana
 Kadhalika Mstahiki Meya wa Kindondoni ndugu Yussuf Mwenda alisema ameguswa sana msiba huu kwani licha Adam kuambiana kuwa msanii lakini pia ni mmsiba wa mwanaharakati mwenzao katika kulitumikia Taifa akiwa na maana ya kwamba ni msiba unaomuhusu Diwani wa Kunduchi Mh. Janeth Rite ambaye ndiye mke wa Marehemu.

Naye Rais Bongo Movie Steve Nyerere kwa masikitiko makubwa aliwataka wasanii wa tasnia hiyo kuacha majivuno na badala yake kuwa na mshikamano na upendo kutokana na hakuna mtu ambaye anaijua siku yake ya kutangulia.

 
Na hii ni nukuu ya Mh. Janeth Rite akimoboleza kwa kusema “ooohh Mume wangu, nakupenda mume wangu, Mungu mpokeee mume wangu Adam, sauti ya mume wangu adam, mpambanaji wangu, askari wangu, nani ataniita my permanent intrest” alisema maneno hayo huku akilia kwa uchungu.
Mke wa marehem Adam Kuambia ambaye pia ni Diwani wa kata ya Kunduchi Mh. Janeth Rite akimuaga mumewe. Mungu ailaze roho ya marehem mahali pema peponi aaaaami.

                                                                                        








No comments:

Post a Comment

Tafadhali Ndugu Msomaji Zingatia Kutumia Maneno mazuri na ya busara kwa Faida ya Wasomaji Wengine