NA
MWANNE OTHMAN
Aliyekuwa
Mpiga Gitaa la Base wa kundi la Jahazi Morden Taarab Juma Mgunda
aliyefariki jana mchana katika Hospitali ya Temeke jijini Dar es
Salaam, hatimaye amezikwa leo katika kijiji cha Mkamba Mkulanga,
imefahamika.
Kwa
Mujibu wa ndugu wa marehemu Juma Mgunda aliyejulikana kwa jina la
Mgeni Saidi ambaye pia ni mpiga kinanda wa Jahazi alisema marehemu
Juma alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya Kifua Kikuu kwa muda mrefu
mara baada ya kuacha bendi ya Jahazi, ambapo aliwahi kutumua dozi na
kumaliza.
![]() |
mwili wa marehemu Juma Mgunda ukiwa ndani ya sanduku tayari kwa kusafirishwa |
Alisema baada ya kupona na kujiona yuko imara akajikuta akirudia kazi zake ngumu za kufanya muziki kusafiri na bendi kama 5stars , na ujana nao akajikuta hali hiyo ya ugongwa ikimrudia kidogo kidogo, huku akiendelea na shuhuli zake, lakini hivi karibuni hali yake ilizidi kuwa mbaya na hatimaye hadi kufikia jana kuiaga dunia.
mwili wa marehemu Juma Mgunda ukiwa ndani ya sanduku tayari kwa kusafirishwa
![]() |
Mtangazaji wa east africa radio na EATV Mwanne Othman akimuhoji mpiga kinanda wa Jahazi Chid Boy |
Juma
Mgunda kabla ya kuingia Jahazi aliwahi kutumikia kikundi cha Tanzania
One Theter yaani TOT na baada ya hapo kwenda Jahazi ambapo alipata
kurikodi albam ya Daktari wa Mapenzi iliyozidi kumuongezea umaarufu
kwa kujulikana kama Juma Mgunda Jino Moja.
Shuhuli
za mazishi hayo yaliyohudhuriwa na wasanii wa bendi mbalimbali za
Taarab na wa maigizo zilianzia nyumbani kwao Tandika na ilipofika saa
5 asubuhi mwili wa marehemu ulisafirishwa kuelekea Mkamba tayari kwa
maziko.
MUNGU
AILAZE ROHO YA MAREHEMU JUMA MGUNDA AAAMIN.
No comments:
Post a Comment
Tafadhali Ndugu Msomaji Zingatia Kutumia Maneno mazuri na ya busara kwa Faida ya Wasomaji Wengine