MAJARIBIO BLOG

Sunday, December 22, 2013

AROBAINI YA NYAWANA KUFANYIKA DISEMBA 29

Arobaini ya aliyekuwa Mwimbaji wa Taarab na mtangazaji wa Taarab radio moja hapa Dar es Salaam Nyawana Issale inatarajiwa kufanyika Disemba 29 mwaka huu nyumbani kwa wazazi wake na mumewe Mwananyamala Kisiwani.

Kwa mujibu wa Kais Mussa Kais ambaye ndiye aliyekuwa Mume wa Marehem NYAWANA alisema kuwa arobaini hiyo ameamua kuifanya yeye kama yeye kwasababu wazazi wake Nyawana tayari walishamfanyia kisomo hicho cha arobaini mnamo tarehe 16.

Kaisi aliomba wadau wa Taarab kutoa ushirikiano kujitokeza kwa wingi katika kufanikisha kisomo hicho cha marehemu mkewe NYAWANA ISSALE FUNDIKIRA

INNALILLAH WAINNA ILAIHI RAAJIUN
MAREHEMU NYAWANA ENZI ZA UHAI WAKE

  MUME WA MAREHEMU NYAWANA  BW.. KAIS MUSA KAIS AKIHOJIWA NA MTANGAZAJI WA EATV NA EAST AFRICA RADIO MWANNE OTHMAN

MWILI WA MAREHEMU NYAWANA UKIWA NDANI YAN SANDUKU LA KUSAFIRISHIA MAITI, AMBAPO ALIZIKWA MKOANI KWAO TABORA

No comments:

Post a Comment

Tafadhali Ndugu Msomaji Zingatia Kutumia Maneno mazuri na ya busara kwa Faida ya Wasomaji Wengine