MAJARIBIO BLOG

Wednesday, December 18, 2013

SAIDA MASHAUZI KUWASHUSHUA WANAOFATILIA NDOA YAKE


Mwimbaji Machachari kwenye tasnia ya Taarab akiwa katika kundi la Mashauzi Classic Saida Ramadhani aka Saida Mashauzi amesema kuwa watu wanaokaa na kumjadili kuhusu yeye na ndoa yake haiwahusun na badala yake waropoke yanayowahusu.

akizungumza na Kipindi cha Tam Tam za Mwambao kinachotangazwa na Mwanne Othman kuopitia east Africa Radio alisema anawashaangaa watu wanaodhani kuwa yeye ameshawishiwa na ndugu zake kutoka kwenye ndoa yake baada ya Mumewe bwana Ramadhan kumkataza kuimba, kitu ambacho ni halmashauri ya kichwa chake ndiyomiliamua bora aendelee kuimba kuliko kumsikiliza mumewe kumkataza kuimba.


Saida alisema kuwa kuimba iko katika damu yake na anaridhika kuona akiwa stejini akifanya vitu vyake huku akisisituiza hata kama hakuna kitu akipatacho lakini nafsi yake inaridhika kuimba./

"Sitaki kuimbi eti kwasababu  mpaka nikijia hapana nataka kuimba kila siku za maisha yangu na ndoa maana nikaamua kurudi kwetu ili niendelee na kazi yangu" alisema Saida wakati akijibu swali ya kwamba kwakuwa bendi ya nyumban si ungemsikiliza mumeo tu anavyotaka, na iwapo siku ukiwa na hamu ya kuimban unaweza kwenda kuimba kwa sababu ni bendi mama.

Pia Saida alisisitiza kuwa kwamba wale  wote wanaojitia kimbelembele kufatilia mambo yake kuizungumzia ndoa yake haijakaa hata miezi minne kwamba waache kwani hakuna yeyote aliyechangia mchango na wale wanaojifanya kwamba wanamjua sana pia waache kwasababu hakuna anayemjua zaidi ya mama mzazi Bi Rukia Jumaa.


Saida akiwa stejini akifanya vitu vyake









Saida siku aliyovalishwa pete ya uchumba aliyekuwa mumewe bwana Rama
Saida siku ya Kitchen Party yake
Saida siku ya  singo party yake

No comments:

Post a Comment

Tafadhali Ndugu Msomaji Zingatia Kutumia Maneno mazuri na ya busara kwa Faida ya Wasomaji Wengine