MAJARIBIO BLOG

Wednesday, April 16, 2014

DIWANI BUJUGO AWAKAKUMBUKA WAHANGA

Na Mwanne Othman


Diwani wa kata ya Magomeni ndugu Julian Bujugo ametoa msaada wa chakula jumla ya magunia 40 ya unga kwa ajili ya kuwasaidia wahanga wa mafuriko wanaoshi katika mtaa wa Sunna Magomeni jiji Dar Salaam.

Akizungumza wakati akiwasilisha msaada huo kwa niaba ya Diwani, Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa huo wa Sunna ndugu Alex Albert alisema anamshkuru Diwani wao kujitolea lakini pia bado wanahitaji misaada zaidi ya chakula ili waweze kujikwamua katika kipindi hiki kigumu walichonacho.


Naye mmoja wahanga hao aliiomba Serikali kufanya upanuzi wa Mto Msimbazi sambamba na Mifereji mikubwa hadi baharini ili kunusuru makazi ya watu ambayo yamekuwa yakiathiriwa na mafuriko.






No comments:

Post a Comment

Tafadhali Ndugu Msomaji Zingatia Kutumia Maneno mazuri na ya busara kwa Faida ya Wasomaji Wengine