MAJARIBIO BLOG

Wednesday, May 28, 2014

MTOTO NASRA AENDELEA VIZURI MUHIMBILI

ATARAJIWA KUHAMISHIWA WODI YA UTAPIAMLO

Na Mwanne Othman

Mtoto aliyetelekezwa huko Morogoro kwa kuweka ndani ya boksi kwa takriban miaka minne anaendelea vizuri katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaa ambapo alifikishwa juzi usiku wa saa 3.

Mwanneothman.blogspot.com leo ilitembelea hospitalini hapo katika jengo la watoto wodi B ambapo ndipo alipolazwa na mtoto huyo na ilipata nafasi ya kuzungumza na Bi Josephine Joel mlezi wa mtoto huyo aliyejitolea kuja nae Dar es Salaam kwa kumpa malezi stahiki, na hapa anaeleze jinsi gani aliweza kumpata mtoto huyo na kuambatana nae hadi Hospitali ya Muhimbili.
mtoto nasra akiwa amekalishwa juu ya meza
 Mwanneothman.blogspot.com ilizungumza na Muuguzi Kiongozi wa wodi hiyo aliyolazwa mtoto huyo Bi Clara Moses ambaye alisema hali aliyokuja nayo tofauti na ya sasa lakini tayari wameshachukua vipimo kwa ajili ya uchunguzi zaidi na leo hii wanatarajia kumuhamishia katika wodi ya Utapiamlo kwa ajili ya kumpatia lishe zaidi.

Hatukuishia hapo pia tulizungumza na wananchi wao kama wazazi wanakizungumziaje kitendo alichofanyiwa mtoto huyo nao ni Katibu Muhtasi wa hospitali ya Muhimbili Bi Jane Mahona na Bwana Abdallah Muhoga mmoja wa kitengo cha Bohari ya dawa hospitalini hapo ambao nao walisema wamesikitishwa sana na kitendo cha unyama aliofanyiwa mtoto huyo.

Mwanneothman.blogspot.com haikutaka kujiridhisha tu kwa kusikia kwamba mtoto huyo anaweza kuongea hivyo ilitumia fursa pekee ya kuweza kuzungumza na mtoto huyo ambaye ilimchukua muda mrefu kujibu pindi alipokuwa akiongeleshwa lakini hatimaye alikweza kujibu maswali aliyokuwa akiulizwa kama vile unaitwa nani, umekunywa nini leo akajibu maziwa amekupa nani bibi.


No comments:

Post a Comment

Tafadhali Ndugu Msomaji Zingatia Kutumia Maneno mazuri na ya busara kwa Faida ya Wasomaji Wengine