MAJARIBIO BLOG

Wednesday, July 2, 2014

Hospitali ya Sinza Lawamani

Na Mwanne Othman

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Sinza ya jijini Dar es Salaam Dokta Benedict Luwoga ametoa wito kwa wateja (wagongwa) ambao wana uthibitisho wa malalamiko ya ya kutotendewa haki yanayoyotokana na uzembe wa wafanyakazi wa hospitali hiyo ili hatua za kinidhamu zichukuliwe juu yao.

Dokta Luwoga ameyasema hayo baada ya hospitali hiyo kuripotiwa kwenye gazeti kuhusu tuhuma mbalimbali zinazoikabili hospitali yake juu ya kumuacha mgonjwa mahututi kwa masaa mawili bila kumpatia huduma ya aina yeyote.

Hapo awali mmoja wa ndugu ambaye amempeleka mgonjwa wake alisema walinzi pia wanachangia kukwaza ndugu wa wagonjwa ambao wakati mwingine huhitajika kumuangalia mgonjwa wake kwa karibu hivyo kujikuta wakifukuzwa na walinzi hap..

Aidha Dr. Luwoga ameviomba kwa vyombo vya habari watumie fursa walizopewa kuweza kuelimisha jamii na si kuleta migongano na kuharibu sifa za vitengo vichache vya Serikali.


hospitali ya sinza katika picha

No comments:

Post a Comment

Tafadhali Ndugu Msomaji Zingatia Kutumia Maneno mazuri na ya busara kwa Faida ya Wasomaji Wengine